ISSRADHANS

Umoja na uzalendo

Umoja na uzalendo

Hot

Post Top Ad

LightBlog

Post Top Ad

Your Ad Spot

Thursday 8 February 2018

Tegete aipa tano alliance

February 08, 2018 0

NA RASHID HASSAN

MENEJA wa zamani wa Uwanja wa CCM Kirumba na mzazi wa mshambuliaji wa soka wa timu ya Maji Maji ya Songea, Jerrson Tegete, Mzee John Tegete, amewapongeza chuo cha kukuza vipaji (academia) ya Alliance ya mwanza kwa kupanda ligi kuu ya Vodacom.

Tegete, alisema ni pongezi na mabadiliko makubwa kwa soka la Tanzania, kwani Alliance walionesha ukomavu mkubwa wa kisoka na kuwa Akademia pekee iliyowahi kupanda ligi kuu bara hapa nchini kwa miaka ya hivi karibuni.

 wachezaji wa Timu ya Alliance
Akizungumza  na mwandishi leo , Mzee Tegete, alisema Alliance imefanikisha ndoto za mkurugenzi wao  ambaye ni Meya wa Jiji la Mwanza , James Bwire, ambapo anaamini watafanikiwa kufanya vizuri kwani wanavipaji vingi ukizingatia wengine wapo chuoni.
Alisema, anaamini Mkurugenzi wa Alliance, atafuata matakwa ya wachezaji wa ligi kuu ya Vodacom, akiwapatia wachezaji wake mikataba pamoja na kuingizwa katika ajira rasmi itakayowawezesha kumudu hali ya kiuchumi iliyopo na familia zao.

“Vijana wamepiga hatua kubwa sana, pamoja na changamoto walionesha nia ya dhati ya kutaka kuingia ligi kuu, nawaomba waendele na umoja wao na mshikamano kama walivyofanya ligi ya FDL, na hakika watafanikiwa na wataitangaza vyema mkoa wa Mwanza na na Taifa kwa ujumla”, alisema Tegete

Mbali na hayo, alimpataka Mkurugenzi wa Alliance, ktafuta wazoefu watakaoongeza morali ya kiushindani licha ya kuwepo na vipaji lukuki lakini haitawasaidia kuhimili mikiki mikiki ya ligi kuu ya Vodacom.

Pia aliitaka TFF, kugeukia Alliance wakati wa uteuzi wa timu ya Taifa na ile ya Vijana kwani anaamini chuo hicho cha vipaji kina vijana wengi wenye uwezo zaidi ya wale wanaoitwa timu ya Taifa na waliokatika ligi kuu ya Tanzania bara.


Alliance FC, ilifanikiwa kupanda ligi kuu bara ikiwa na alama 28 kwenye kundi ‘C’ nyuma ya Biashara ya mara ambao walikuwa kinara wa kundi hilo.
Read More

"KMC kufanya kongamano kupongeza wachezji na maandalizi"

February 08, 2018 0
NA YUSUPH MWAMBA

TIMU ya Soka ya Kinondoni Municipal Council (KMC), yenye maskani yake Wilaya ya Kinondoni imeandaa kongamano rasmi kwa ajili ya kuwapongeza wachezaji wake mara baada ya kufanikiwa kukata tike ya kupanda  Ligi kuu Tanzania bara msimu ujao.


Kongamano hilo linatarajiwa kufanyika tarehe 9 mwezi Februari, 2018 Siku ya Jumamosi   kwenye Uwanja wa Biafra kuanzia  majira ya saa 8:oo mchana.

Akizungumza na mwandishi,  Mwenyekiti wa Klabu  hiyo, Suzan Massawe,  alisema kongamano hilo ni moja ya furaha na hamasa kwa timu ya KMC kupanda ligi kuu bara kwani wataongeza morali ya ushindani na hali ya kujituma.


Alisema kongamano hilo linatarajia kuanza  mishale ya saa 6 mchana ambapo gari la matangazo litazunguka na wachezaji wa KMCkatika meneo mbali mbali ndani ya wilaya ya Kinondoni   kisha saa 8 mchana watawasili Uwanja wa Biafra tayari kwa kukamilisha kongamano hilo.

 “Huu ni utaratibu, tunawapongeza sana KMC kwani walifanya kile tulichowatuma wametubeba hatuna budi ya kuwapongeza jambo ambalo litawapa  morali ya ushindani na hali ya ushindi watakapoingia kwenye kivumbi cha ligi kuu msimu ujao”, alisema Suzan

Naye Mwenyekiti na mmiliki wa Timu ya soka ya Kinondoni FC, Saleh Alawi, aliwapongeza KMC  na kuwataka wajenge ushirikiano  imara na kujengeka kifikra katika kuelekea kwenye kinyang’anyiro cha Vodacom ambako kunaonekana kuwa na ushindani mkubwa tofauti na ligi daraja la kwanza.

KMC ambayo ilikuwa kundi C ilifanikiwa kupanda ligi kuu baada ya kujikusanyia alama 28 ikifuatiwa na Biashara ya Mara. 
Read More

Mgagani: Ni Mboga, Kinga, Tiba, Sabuni, Mafuta na Mashudu

February 08, 2018 3
NA ODRIAN NICOLAUS
LABLA kwa sababu ya ladha chungu ya mboga ya majani aina ya mgagani watu wengi hukimbilia kula mchicha na mboga zingine za majani ambazo hazina ladha hiyo.
Related image
Mmea wa mgagani  unavyoonekana  (pichani)
Ingawa wataalamu wanasema wanaofanya hivyo wanakimbia kinga na tiba ya maradhi mbalimbali, achilia mbali kwamba pamoja na kinga na tiba, mbegu na mizizi vinaweza kukamuliwa na kusafishwa kisha mbegu hizo  hutoa mafuta yanayotengeza sabuni, nishati ya bio-fuels na bidhaa zingine.

Mmea huo huota sehemu yoyote yenye udongo wa rutuba na tifutifu hasa kwenye mabonde, nyumba zilizohamwa (pagala) na maeneo mengine kama hayo. Bado inaaminika na wengi kuwa ni mboga ya watu masikini.
Ingawa kadri ya mahitaji ya tiba na lishe kila uchao, baadhi ya watu hasa katika ukanda wa Pwani wameanza kuchukua mbegu zake na kuzisia kama mchicha na mboga zingine za majani kwa ajili ya chakula, dawa, biashara ya kuchuuza na matumizi mengine.
ASILI YA MGAGANI:
Historia inaonyesha kwamba asili ya mmea wa mgagani ni Afrika Mashariki. Kutokana na mwingiliano wa watu, ndege na wayama ulienea hadi Ethiopia, Somalia, Asia Kusini na Amerika nazo kujumuishwa kama nchi zinazoasisi mmea huo.
Kwa mwingiliano huohuo, mmea huo uliendelea kusambaa katika nchi zote za kitropiki barani Afrika, Asia na Amerika kama anavyobainisha Dk. Edger Kapagi wa kliniki ya Mazingira Natural Products ya jijini  Mbeya.

Anasema ni mboga muhimu na inayothaminiwa mno na watu wa Bara la Asia (Wahindi na Wathai (Thailand) kutokana na watu wa jamii hizo kuwa kwanza duniani kutumia mmea hio kiafya ingawa asili  yake ni Afrika Mashariki ulikokuwa mboga zaidi.

Mgagani kama unavyotambulika kwa jina la kibotania,  cleome gynandra hujulikana na Waingereza kwa  majina ya African Cabbage, spider wisp, cats whisker, spider plants, na bastard mustards.

Huko Ufaransa, Wafaransa wanauita caya blanc, br’ede caya na mouzambe. Kiswahili jina maarufu ni mgagani ingawa yapo makabila kama vile wasambaa huuita mkabili shemsi na mwangani mgange.

Akizungumzia juu ya umuhimu wa mboga hiyo umesheheni virutubisho vingi na a madini ya beta carotene, vitamin C, Chuma, Magnesium, calcium na phosphorus, protini na amino acid nyingi, anasema Dk. Kapagi.

KUHUSU TIBA, KINGA:
Anasema ni kinga dhidi ya maradhi nyemelezi kwa watoto na watu wazima. Huukinga mwili na magonjwa ya kisukari, saratani na moyo, hutibu maumivu ya kichwa, kufunga choo, maumivu ya tumbo, kuzuia kutapika.

Zaidi;  anasema huzuia na kutibu homa ya naimonia (pneumonia),  maumivu ya sikio, bawasiri, maumivu ya hedhi kwa wanawake kwa ulaji wa mara kwa mara. Pia hutibu uvimbe katika kizazi cha mwanamke, jongo (gout) na anemia. 

“Mgagani unafaa kwa mama wajawazito wanaotaka kujifungua kwani huiandaa njia ya uzazi kupitisha mtoto na hivyo kumpunguzia maumivu mama husika (labor pains ) na kuongeza nguvu mwilini, kutoka maziwa kwa wingi, ya kutosha kwa mtoto kunyonya,”anasema na kuendelea...

Mizizi hutibu homa, kuumwa na n'ge na nyoka. Lakini ni mboga nzuri kwa waliotoka tohara kwani huongeza damu haraka iliyotoka wakati wa kutahiriwa. 
FAIDA ZA MGAGANI KIUCHUMI:
Mbegu zake zinaweza kukamuliwa na kusafishwa. Mafuta yake hutumika kutengeneza sabuni, bio-fuels na vitu vingine. Majani na mbegu ni chakula kizuri kwa ajili ya kuku na ndege wengine, ng’ombe, ngamia, farasi na wanyama wa porini wanaofugwa.

Ndiyo maana watu wengi wa ukanda wa Pwani ameanza kulima bustani za mmea wa mgagani na kuuza. Watu walioelekezwa matumizi yake wameanza kununua kwa wingi na kula kama mboga wakati huohuo kinga na tiba pia.

MATUMIZI:
Mkulima anaweza kumshauri mteja wake namna bora ya kupunguza uchungu wakati wa kuipika ili kumhamasisha mteja wake. Kutokana na lagha ya uchungu unaweza kumpoteza au kupunguza wateja, badala yake mlaji anashauriwa kuchanganya mgagani na tui la karanga ili kupunguza uchungu.

Kula kadri inavyofaa kama mboga zingine za mezani. Ni muhimu pia kuzingatia ushauri wa kitaalamu na kuanza kuchukulia mboga hii kama mkombozi wa afya, anasema Dk. Kapagi.
Read More

Jini Kabula bado yupo yupo kwanza

February 08, 2018 0


Miriam Jolwa maaru ‘Jini Kabula’

NA YUSUPH MWAMBA

MSANII mwenye uwezo mkubwa na ubunifu nchini, kwenye tasnia ya Bongo Muvi kutoka Tamthiliya ya Jumba la Dhahabu, Miriam Jolwa maarufu kama ‘Jini Kabula’ amesema kuwa kwa sasa hana mpango wa kuiigiza badala yake anajiwekeza kwenye ujasiriamali.

Kabula,ambaye hivi karibuni alizua taharuki baada ya kupatwa ugonjwa ambapo kwa sasa hali yake inakwenda vizuri na afya yake imeimarika.

Akizungumza na mwandishi Kabula, alisema sio kwamba ameachana na sanaa moja kwa moja lakini ameona akae pembeni ili kuangalia upepo mwingine ambako kwa sasa amejielekeza kwenye masuala ya ujasiriamali.

“Nipo poa kwa sasa namshukuru Mungu , afya yangu imeimarika, kikubwa kwa sasa nipo nje ya sanaa, lakini sijaiacha kabisa nafanya biashara zangu upepo ukikaa sawa nitarudi ila najua hakuna atakaechukua nafasi yangu kwakuwa kabula ni mbunifu na mtu makini katika kazi zake”, alisema

Msanii huyo, aliyewahi kutamba kupitia Tamthilia ya  Jumba la Dhahabu , yupo mbioni kuzindua nembo ya biashara  zake anazoziendesha japo hakutaka  kuziweka hadharani.


Read More

Shilole awataka wasanii wapambane na hali zao

February 08, 2018 0
NA ISSA RAMADHANI

MSANII wa miondoko ya pwani hapa nchini Zena Yusuf Mohammed  maarufu “ Shilole” , amesema wasanii wanatakiwa kufanya kazi kwa bidii ili kukabiliana na hali ya kiuchumi iliyopo.

Shilole,  ambaye hivi karibuni alifunga ndoa na muwewe Uchebe, aliwataka wasanii wakaze buti na kuangalia fursa zilizopo ili kukabiliana na hali ya uchumi, kwani sanaa ya sasa ni ngumu ukilinganisha na  miaka iliyopita.



Akizungumza na mwandishi, Shilole , alisema mwaka jana soko la sanaa lilikuwa zuri ukilinganisha uchumi ulikuwa unaoneka tofauti sasa ambako kila msanii anatakiwa ajitume na kupambana na hali yake katika kujitengenenezea maisha yake na familia yake.

“Muziki wa sasa sio wa kubweteka, lazima ujitume, utengeneze nyimbo nzuri zitakazo wavutia mashabiki kama msanii atatoa ngoma mbaya basi hali ya kiuchumi itaendelea kuyumba kila siku”,alisema Shilole

Alisema kuwa, wasanii walikuwa wakitegemea sana shoo za  nje na za ndani, ila kwa sasa hali ni tofauti wananchi hawana fedha za kuingia kwenye kumbi za starehe, watu wengi wanafikiria jinsi ya kuhudumia familia zao kuliko starehe, hivyo kama wanataka pesa ni lazima wafanye kazi nzuri zitakazowavutia mashabiki.

Aidha, Shilole, yupo mbioni kuachia nyimbo ambayo hakumshirikisha mtu lakini aliweka bayana kwamba ngoma hiyo itatarajia kutoka  kati kati ya Februali mwaka huu, hivyo mashabiki wake wakae mkao wa kula.


Read More

YAJUE MAMBO YANAYOSABABISHA MAHUSIANO KUVUNJIKA

February 08, 2018 0
KWA mara nyingine nakukuribisha msomaji  katika safu hii ya mahusiano ili tuweze kubadilishana mawazo na kuelimishama kuhusu masuala mbalimbali yanayohusiana na ndoa na uchumba, mafanikio na changamoto zake.
Leo tutazungumzia mambo ya kufanya ili kuboresha ndoa  au mahusiano kwa kuyajua mambo yanay sababisha mahusiano ya kimapenzi kuvunjika.
NA ISSA RAMADHANI
Tabia hizi ndizo zinasababisha mahusiano ya watu wengi kuvunjika, hata ndoa kuharibika baada ya kukosekana uvumilivu. Hali hiyo husababisha maumivu, vidonda vya mapenzi na hata vifo na kuwafanya watu wengine kuchukia kupenda au kupendwa katika maisha yao.
Mawasiliano duni
Kutokuwa na mawasiliano ya karibu na mwenzi wako, husababisha matatizo kujitokeza pia         ukishindwa kukaa na kujadili mfano kumpigia simu, kuonana, kutoka “out” na kuzungumza ili kupata ufumbuzi ndio mwanzo wa kuachana na mwenzi wako, huwa si lazima akuambie utaona mazingira yanabadilika na mwisho mnaachana.
Maelewano
Hili ni jambo jema ni muhimu kwa afya ya ndoa au uchumba wenu. Kuwa tayari muda wote kumsikiliza mwenzako anachozungumza.Baada ya ratiba ngumu za siku kuwa na hamu ya kumsikiliza mwenzako na kumuuliza maswali mbalimbali.kumbuka wakati mwinginemke au mume wako anahitaji kukuuliza au kukusikiliza, epuka sana kutoa hitimisho wewe tu!, fungua masikio yako na msikilize kile anachosema mwenzako.

Kujali

Hapa kuna shida sana, wapo baadhi ya wapenzi wamo kwenye mahusiano lakini hawajali maumivu ya mwenzie. Mfano anumwa, anamatatizo au huzuni hiki ndio kipindi cha kukaa na kumliwaza, lakini asilimia kubwa sana wako “busy” na mambo yao.
Ubishi
Tabia hii hivi sasa inashika kasi sana kwenye mahusiano mengi. Hata katika jambo ambalo kueleweshana lazima kuwe na ubishi usiokuwa na tija. Kwa mke na mume kushindwa kuelewana huharibu uhusiano. Kila mmoja ajaribu kujishusha ili kupata muafaka katika jambo mlilotofautiana. 
Kutokubali makosa
Hakika utakubaliana na mimi kuwa baadhi ya wapenzi wana tatizo hili la kutokubali kosa na kujisahihisha japo kuna ushaidi. Kukubali makosa, kuomba msamaha na kujisahihisha na jambo zuri katika kuimarisha mahusiano. 
Kutoonesha upendo
Onyesha unampenda sana mke au mume wako daima. Kila siku hakikisha unadhihirisha upendo wako kwake usichoke. Mbusu mke au mume wako, mkumbatie kila mara kama ishara ya upendo. Kama mtapendana kwa dhati basi bila shaka mtaheshimiana na kila mmoja atamthamini mwenzake. kila siku tafakari kwa nini ulimpenda yeye tu na wala si mwingine, hii itakufanya umpende zaidi mke au mume wako.
Kutikuwa muwazi

Kukaa na kuelezana mambo unayopenda na usiyoyapenda kwa mwenzi wako kwenye mahusiano ni jambo zuri kwani husababisha kujua nini  ukimfanyia mwenzio anakuwa na furaha na nini kina mkera. Kuwa muwazi katika mipangoya  kustawisha mahusiano yenu na maendeleo kwa kushirikishana.
Kustahiana
Kitendo cha kumgombeza mwenzi wako mbele za watu kinaonyesha picha mbaya mnavyoishi  kwa jamii inayowazunguluka.Wapo badhi ya wapenzi bila kupishana kauli  hajisikii raha. Kila mtu hapendi malumbano, ugomvi na kudhalilishwa. 

Mthamini mwenzako
Kila mmoja anapaswa kutambua thamani ya mwenzi wake katika maisha. Mnapaswa kuelewana  na kujuana tabia zenu ili kujenga maisha bora ya mapenzi yenu. Mzungumze kwa lugha upole na upendo. 
Shugulikia matatizo yako yanayokusumbua kwani hapa dunia kila binadamu aliyekamilika  anitaji kuwa na mke, mume na hatimaye familia. Badilika sasa.


Read More

Wednesday 20 December 2017

Kampeni ya kuhamasisha Tohara,elimu kwa Vijana wa Kiume Kuanzishwa

December 20, 2017 0
 Kampeni ya Kuhamasisha Tohara kwa Vijana wa Kiume Kuanzishwa



MBEYA.
VIJANA WA KIUME wametakiwa kuwa tayari kufanyiwa tohara ili kukabiliana na maambukizi ya magonjwa ya zinaa.

Aidha Mkurugenzi Mtendaji wa asasi isiyokuwa ya kiserikali ya Sauti ya Mama Afrika (Samofa), Thabitha Bughali alisema jana kuwa, wameanza kampeni kuhamasisha tohara kwa vijana walio na miaka 12 katika shule za msingi na sekondari kwa lengo la kupunguza kasi ya maambukizi ya virusi vya Ukimwi.

Alisema katika kampeni hiyo wanawalenga vijana wa umri huo kutokana na changamoto ya utandawazi katika jamii na wengi wao kujihusisha na ngono wakiwa na umri mdogo na hivyo kuwa katika hatari ya kupata Ukimwi.

Bughali alisema kuanzia Januari hadi Julai, wamefanya uhamasishaji kwa vijana 500 katika baadhi ya shule za kata za Utengule Usongwe na Nsalala, Mbeya Vijijini.

Mkazi wa Itende, Joshua Seme alisema ili Serikali ifanikiwe katika kampeni ya tohara, elimu zaidi inapaswa kutolewa maeneo ya vijijini ambako kuna changamoto ya idadi kubwa ya wanaume wasiofanyiwa tohara.

Desemba 6, mkuu wa mkoa wa Mbeya, Amos Makalla aliwaagiza waganga wakuu wa hosptali mkoani hapa kufanya kila linalowezekana ili kupunguza maambukizi ya virusi vya Ukimwi.

Agizo hilo alilitoa katika kikao cha afya mkoa kilichohusisha wakuu wa wilaya, wakurugenzi wa halmashauri, waganga wakuu na wataalamu wa afya. 

Read More

Post Top Ad

Your Ad Spot