YAJUE MAMBO YANAYOSABABISHA MAHUSIANO KUVUNJIKA - ISSRADHANS

Umoja na uzalendo

Umoja na uzalendo

Hot

Post Top Ad

Your Ad Spot

Thursday 8 February 2018

YAJUE MAMBO YANAYOSABABISHA MAHUSIANO KUVUNJIKA

KWA mara nyingine nakukuribisha msomaji  katika safu hii ya mahusiano ili tuweze kubadilishana mawazo na kuelimishama kuhusu masuala mbalimbali yanayohusiana na ndoa na uchumba, mafanikio na changamoto zake.
Leo tutazungumzia mambo ya kufanya ili kuboresha ndoa  au mahusiano kwa kuyajua mambo yanay sababisha mahusiano ya kimapenzi kuvunjika.
NA ISSA RAMADHANI
Tabia hizi ndizo zinasababisha mahusiano ya watu wengi kuvunjika, hata ndoa kuharibika baada ya kukosekana uvumilivu. Hali hiyo husababisha maumivu, vidonda vya mapenzi na hata vifo na kuwafanya watu wengine kuchukia kupenda au kupendwa katika maisha yao.
Mawasiliano duni
Kutokuwa na mawasiliano ya karibu na mwenzi wako, husababisha matatizo kujitokeza pia         ukishindwa kukaa na kujadili mfano kumpigia simu, kuonana, kutoka “out” na kuzungumza ili kupata ufumbuzi ndio mwanzo wa kuachana na mwenzi wako, huwa si lazima akuambie utaona mazingira yanabadilika na mwisho mnaachana.
Maelewano
Hili ni jambo jema ni muhimu kwa afya ya ndoa au uchumba wenu. Kuwa tayari muda wote kumsikiliza mwenzako anachozungumza.Baada ya ratiba ngumu za siku kuwa na hamu ya kumsikiliza mwenzako na kumuuliza maswali mbalimbali.kumbuka wakati mwinginemke au mume wako anahitaji kukuuliza au kukusikiliza, epuka sana kutoa hitimisho wewe tu!, fungua masikio yako na msikilize kile anachosema mwenzako.

Kujali

Hapa kuna shida sana, wapo baadhi ya wapenzi wamo kwenye mahusiano lakini hawajali maumivu ya mwenzie. Mfano anumwa, anamatatizo au huzuni hiki ndio kipindi cha kukaa na kumliwaza, lakini asilimia kubwa sana wako “busy” na mambo yao.
Ubishi
Tabia hii hivi sasa inashika kasi sana kwenye mahusiano mengi. Hata katika jambo ambalo kueleweshana lazima kuwe na ubishi usiokuwa na tija. Kwa mke na mume kushindwa kuelewana huharibu uhusiano. Kila mmoja ajaribu kujishusha ili kupata muafaka katika jambo mlilotofautiana. 
Kutokubali makosa
Hakika utakubaliana na mimi kuwa baadhi ya wapenzi wana tatizo hili la kutokubali kosa na kujisahihisha japo kuna ushaidi. Kukubali makosa, kuomba msamaha na kujisahihisha na jambo zuri katika kuimarisha mahusiano. 
Kutoonesha upendo
Onyesha unampenda sana mke au mume wako daima. Kila siku hakikisha unadhihirisha upendo wako kwake usichoke. Mbusu mke au mume wako, mkumbatie kila mara kama ishara ya upendo. Kama mtapendana kwa dhati basi bila shaka mtaheshimiana na kila mmoja atamthamini mwenzake. kila siku tafakari kwa nini ulimpenda yeye tu na wala si mwingine, hii itakufanya umpende zaidi mke au mume wako.
Kutikuwa muwazi

Kukaa na kuelezana mambo unayopenda na usiyoyapenda kwa mwenzi wako kwenye mahusiano ni jambo zuri kwani husababisha kujua nini  ukimfanyia mwenzio anakuwa na furaha na nini kina mkera. Kuwa muwazi katika mipangoya  kustawisha mahusiano yenu na maendeleo kwa kushirikishana.
Kustahiana
Kitendo cha kumgombeza mwenzi wako mbele za watu kinaonyesha picha mbaya mnavyoishi  kwa jamii inayowazunguluka.Wapo badhi ya wapenzi bila kupishana kauli  hajisikii raha. Kila mtu hapendi malumbano, ugomvi na kudhalilishwa. 

Mthamini mwenzako
Kila mmoja anapaswa kutambua thamani ya mwenzi wake katika maisha. Mnapaswa kuelewana  na kujuana tabia zenu ili kujenga maisha bora ya mapenzi yenu. Mzungumze kwa lugha upole na upendo. 
Shugulikia matatizo yako yanayokusumbua kwani hapa dunia kila binadamu aliyekamilika  anitaji kuwa na mke, mume na hatimaye familia. Badilika sasa.


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot