NA
ISSA RAMADHANI
MSANII
wa
miondoko ya pwani hapa nchini Zena Yusuf Mohammed maarufu “ Shilole” , amesema wasanii
wanatakiwa kufanya kazi kwa bidii ili kukabiliana na hali ya kiuchumi iliyopo.
Shilole, ambaye
hivi karibuni alifunga ndoa na muwewe Uchebe, aliwataka wasanii wakaze buti na
kuangalia fursa zilizopo ili kukabiliana na hali ya uchumi, kwani sanaa ya sasa
ni ngumu ukilinganisha na miaka
iliyopita.
Akizungumza na mwandishi, Shilole , alisema mwaka jana
soko la sanaa lilikuwa zuri ukilinganisha uchumi ulikuwa unaoneka tofauti sasa
ambako kila msanii anatakiwa ajitume na kupambana na hali yake katika
kujitengenenezea maisha yake na familia yake.
“Muziki wa sasa sio wa kubweteka, lazima ujitume, utengeneze
nyimbo nzuri zitakazo wavutia mashabiki kama msanii atatoa ngoma mbaya basi
hali ya kiuchumi itaendelea kuyumba kila siku”,alisema Shilole
Alisema kuwa, wasanii walikuwa wakitegemea sana shoo
za nje na za ndani, ila kwa sasa hali ni
tofauti wananchi hawana fedha za kuingia kwenye kumbi za starehe, watu wengi
wanafikiria jinsi ya kuhudumia familia zao kuliko starehe, hivyo kama wanataka
pesa ni lazima wafanye kazi nzuri zitakazowavutia mashabiki.
Aidha, Shilole, yupo mbioni kuachia nyimbo ambayo hakumshirikisha
mtu lakini aliweka bayana kwamba ngoma hiyo itatarajia kutoka kati kati ya Februali mwaka huu, hivyo
mashabiki wake wakae mkao wa kula.
No comments:
Post a Comment