HEKA
HEKA zikiendelea za usajili,Timu nyingine za Ligi Kuu Tanzania Bara zikiwa
kwenye mchakato wa kuimalisha vikosi vyao ikwa ni maandalizi ya ligi, Kocha wa
Yanga, George Lwandamina, amesema
usajili watakaoufanya ni kwa ajili ya michuano ya Ligi ya Mabingwa
inayoandaliwa na Shirikisho la Soka Afrika (CAF).
Ambapo ,Yanga itashiriki michuano hiyo mikubwa Afrika kwa ngazi ya klabu kuanzia Februari mwakani.
Kikosi cha Yanga kinampango wa kusajili wachezaji watatu kwenye safu ya ulinzi, kiungo na ushambuliaji.Akizungumza jijini Dar es Salaam, Lwandamina, alisema kwa sasa ni wakati wa kujipanga kwa ajili ya michuano ya kimataifa.
“Nina kikosi kizuri, lakini kwa michuano ya kimataifa ni lazima tuongeze wachezaji kwa ajili kupambana kwenye michuano hiyo, tunataka kuona tunafanya vizuri,” alisema Lwandamina.
Kimsingi Lwandamina, alisema kuwa yapo
mapendekezo aliyoyawakilisha kwa uongozi wa timu hiyo ambapo ameeleza wachezaji
wanaopaswa kuongezwa kwenye kikosi chake.Ambapo ,Yanga itashiriki michuano hiyo mikubwa Afrika kwa ngazi ya klabu kuanzia Februari mwakani.
Kikosi cha Yanga kinampango wa kusajili wachezaji watatu kwenye safu ya ulinzi, kiungo na ushambuliaji.Akizungumza jijini Dar es Salaam, Lwandamina, alisema kwa sasa ni wakati wa kujipanga kwa ajili ya michuano ya kimataifa.
“Nina kikosi kizuri, lakini kwa michuano ya kimataifa ni lazima tuongeze wachezaji kwa ajili kupambana kwenye michuano hiyo, tunataka kuona tunafanya vizuri,” alisema Lwandamina.
“Najua uongozi unafanyia kazi ripoti yangu, ni lazima pia kuangalia michuano ya kimataifa na ukiangalia tumebakiza Januari tu kabla ya kuanza michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika,” alisema Lwandamina.
Aidha, Lwandamina, alisema katika ripoti hiyo ameelezea pia ni wachezaji gani ambao uongozi haupaswi kuwaachia waondoke.
Kikosi cha Yanga kinaendelea na mazoezi kwenye Uwanja wa Uhuru kujianda na michezo ya Ligi Kuu ambapo mchezo unaofuata watacheza na Mbao FC kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
No comments:
Post a Comment