"LWANDAMINA ALETEWA STRIKER NOMA WA KIMATAIFA" - ISSRADHANS

Umoja na uzalendo

tanzania

Hot

Post Top Ad

Monday, 11 December 2017

"LWANDAMINA ALETEWA STRIKER NOMA WA KIMATAIFA"

Your Ad Spot


 .com/blogger_img_proxy/
 yanga wakiwa mzoezini

WAKATI  zimebaki siku nne tu kabla ya dirisha dogo la usajili kufungwa Desemba 15,nchini  Kocha wa YangaGeorge Lwandamina leo Jumatatu anatarajia kupokea jina la mshambuliaji raia wa DR Congo kutoka kwa mwenyekiti wa usajili wa timu hiyo, Hussein Nyika, ambaye alikuwa nje ya mipaka ya Tanzania, kwa ajili ya kusaka mshambuliaji.

Ambapo Nyika alitembelea nchi ya Ghana, Congo na Burundi lengo ni kutafuta mshambuliaji wa kimataifa ambaye atajiunga na timu hiyo kwa ajili ya kuongeza nguvu kutokana na washambuliaji wa kutumainiwa Amissi Tambwe na Donald Ngoma kuwa majeruhi jambo ambalo limesababisha kuwategemea Ibrahim Ajibu na Mzambia, Obrey Chirwa pekee.

Hata hivyo ,Chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya Klabu Yanga kimesema kuwa Nyika anatarajiwa kukutana na Lwandamina kwa ajili ya kumpa ripoti juu ya aina gani ya mshambuliaji ambaye anaweza kujiunga na timu hiyo baada ya kufanya uchunguzi kwenye nchi za Congo, Ghana na Burundi ambapo alienda kwa lengo la kusaka mshambuliaji.
.com/blogger_img_proxy/
 Kocha wa YangaGeorge Lwandamina
“Leo Jumatatu, mwenyekiti wetu wa usajili, Hussein Nyika anatarajia kufanya kikao na kocha, Lwandamina kwa ajili ya kumpa mrejesho wa kile ambacho amekutana nacho baada ya kwenda nje kusaka mshambuliaji ambaye kocha anamuhitaji kabla ya dirisha kufungwa.ili kuendelea kwa ligi kuu Tanzania bara “VPL”

“Hadi sasa kuna majina ya washambuliaji watatu kutoka nchi za DR Congo, Ghana na Burundi ambapo alienda wiki chache zilizopita kwa ajili ya kuangalia ni nani ambaye anaweza kuwa msaada katika kipindi hiki ambacho fowadi yetu imepungua makali kutokana na baadhi yao kuwa majeruhi,” kilisema chanzo hicho.

Hata hivyo, alipotafutwa Nyika ili aweze kuzungumzia hilo, hakuweza kupatikana kutokana na simu yake ya mkononi kuita tu bila ya kupokelewa.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad