Benki ya Mkombozi yawa mkombozi wenye VVU - ISSRADHANS

Umoja na uzalendo

Umoja na uzalendo

Hot

Post Top Ad

Your Ad Spot

Monday, 11 December 2017

Benki ya Mkombozi yawa mkombozi wenye VVU



 Image result for jengo la mkombozi bank
NA GEORGE MSHANA
DAWATI   linaloshughulikia mikopo kwa wateja wanaoishi na Virusi vya Ukimwi (VVU) la Benki ya Mkombozi (Mkombozi Bank) limewashauri watu wanaoishi na Virusi vya Ugongwa wa Ukimwi kuwa na utamaduni wa kujiwekea akiba kwa kufungua akauti ili kuwa sifa ya kupata mkopo badala ya baadhi yao kukata tamaa.
 
Afisa Maendeleo ya Jamii wa Benki hiyo, Rose Mpeleta pia aliwashauri kujiunga kwenye vikundi ili kuungwanishwa na mifuko ya hifadhi ya jamii ili kupitia mfumo huo waweze kupata matibabu kwa kadi za mifuko hiyo au ya Bima ya Afya (NHIF).
Related image
Alisema dawati hilo limeanzishwa mahususi kwa  kundi hilo kutoa  mikopo ya riba nafuu  ingawa tathimini inaonesha kiwango cha wanaopewa mikopo hakiridhishi ukilinganisha na hali halisi, hivyo  kutoa ushauri kwa wahusika kuchangamkia fursa hiyo.

“Kiasi ambacho kila mteja kwenye kikundi anaweza kupata kinaanzia 300,000/-… mteja anaweza kupata mkopo wa miezi mitatu hadi  tisa kwa riba ya  asilimia 2.5 tu.  Marejesho hufanyika baada ya miezi mitatu. Mteja anaweza kupata mkopo bila kuwa na dhamana isiyohamishika,” alisema Mpeleta.

Alisema tofauti na benki zingine, mteja huandalia kabla kukopa ikiwa ni pamoja na kufundishwa katika madarasa maalimu mbinu mbalimbali za kibiashara kama vile kutunza kumbukumbu za hesabu, sababu na umuhimu wa kukopa, kufungua akauti, nidhamu ya mkopo, umuhimu wa marejesho na madhara ya kukopa na kutorejesha.

Kwa kutumia mfumo huo alisema wafanyabiashara na wajasiriamali wadogo na wakati wanaofanya biashara katika mfumo rasmi na usiokuwa rasmi wameweza kukopa na kuendesha biashara zao na kurejesha bila kusuasua. 

Hiyo pia ni mikopo hiyo kutolewa kwa masharti nafuu kama vile riba ndogo na benki hiyo kutokuwa na  sharti gumu la  dhamana isiyohamishika kama vile nyumba. “Lengo letu ni kuwakwamua watu kiuchumi kwa asilimia 100,” alisema.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot