NA
GEORGE MSHANA
WAFANYABIASHARA hapa nchini
wameshauriwa kuwa alama kuthaminisha biadhaa (Barcode) ili kuzifanya bidhaa zao kuuzwa katika masoko
makubwa ya ndani na nje ya nchi.
Ili
kufikia malengo Taifa la Uchumi wa Kati kwa njia ya biashara na viwanda.
Ushauri
huo ulitolewa jijini Dar es Salaam na Afisa Masoko wa Kampuni ya Global
Standard 1 (GS1 Tanzania) Musa Fundi katika mahojiano maalumu na gazeti hili na
kufafanua kuwa baadhi ya wafanyabishara hushindwa kufikia ndoto za kibiashara
kwa kutojua umuhimu wa nembo hiyo na ya Shirika la Viwango (TBS) katika
kuongeza wateja.
“Wafanyabiashara wengi hawana mtazamo kuuza
bidhaa zao ngazi ya kimataifa…wakati mwingine ni kwa kutojua mbinu za kufika
huko. Hata baadhi ya nembo muhimu kama barcode hawajui umuhimu wake...tumeanza
kutoa mafunzo haya kwa kushirikianana Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo Vidogo
(SIDO),”alisema Fundi.
Alisema
pia GS 1 wameanza kuelekeza wajasiriamali na wafanyabiashara wadogo namna bora
ya kufungasha bidhaa, umuhimu wa nembo zinazoonesha nembo ya ubora, mwisho wa
matumizi ya bidhaa kwani mambo hayo ni muhimu kwenye bidhaa hasa
katika soko la kimataifa.
Afisa
Masoko huyo aliongeza kwa kusema kuwa shirika lake limeingia makubaliano na Shirika
la Viwango (TBS) kuhamasisha
wafanyabiashata kuwa na Barcode kabla ya kuomba kusajili upya alama ya TBS
katika bidhaa husika.
“Ni
agizo la Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji
kufuatia barua ya waziri mwenye dhamana nkuwashauri wajasiriamali watumie barcode
ya Tanzania. Hii itasaidia mnunuzi ajue kuwa hiyo bidhaa imetoka na
imetengenezwa Tanzania,”alisema.
Alisema
bidhaa nyingi za hapa nchini zimewekwa nembo hiyo kutoka Kenya na Afrika Kusiwakati ukweli ni kwamba imezalishwa Tanzania. Hivyo kwa sasa lazima
kila bidhaa ijulikane imetengenezwa
Tanzania, lazima iwe na barcode ya Tanzania, alisisitiza.
Fundi
alisema kupitia serikali za mitaa mbalimbali,
jumla ya wajasiriamali 19,800 wanatarajiwa kupatiwa nembo ya Barcode kufikia
mwishoni mwa mwaka. Hadi sasa 16,800
wamekwishapatiwa.
“Tunaendelea
kutoa elimu kwa umma kuhusu umuhimu huu, ambapo wengi wamebadilika na baada ya
kuina mafanikio kwa wengine,”alisema.
GS1
Tanzania ilianzishwa kwa malengo ya kutoa bar code kwa wajasiriamali ambao wanazalisha bidhaa mbalimbali. Bar code
inayowekwa kwenye bidhaa zao, inawasaidia bidhaa hizo ziweze kuuzwa kwenye
masoko makubwa na kwenye masoko ya kimataifa.
No comments:
Post a Comment