SIMBA YAIZIDI MBINU YANGA, MO ASAINI MIAKA 2 SIMBA SC. - ISSRADHANS

Umoja na uzalendo

Umoja na uzalendo

Hot

Post Top Ad

Your Ad Spot

Monday, 11 December 2017

SIMBA YAIZIDI MBINU YANGA, MO ASAINI MIAKA 2 SIMBA SC.



 
KLABU ya Yanga imeshindwa kumpa kiungo Mohamed Ibrahim ‘Mo Ibra’ kile anachotaka, hivyo leo Jumatatu mchezaji huyo anatarajiwa kusaini mkataba wa miaka miwili na klabu yake ya Simba.

Akizungumza na Championi Jumatatu, Meneja wa Mo, Jamal Kisongo amesema kuwa mteja wake huyo anatarajiwa kusaini mkataba wa miaka miwili na Simba baada ya kushindwana na Yanga ambao nao walikuwa wanamtaka huku Msimbazi wao wakitimiza makubaliano waliyokuwa wanataka.

Alisema walifanya mazungumzo na Yanga lakini kuna baadhi ya vitu kwenye mkataba hawakuridhika navyo na walipozungumza na Simba wakakubali kurekebisha baadhi ya vipengele kwenye ule mkataba wa awali hivyo rasmi mteja wake anabaki Simba na leo atasaini kandarasi baada ya ile ya awali kumalizika.


 Image result for Mohamed Ibrahim  mchezaji wa simba

“leo natarajiwa kwenda kusaini mkataba mpya wa miaka mawili na mchezaji Mohammed pale Simba baada ya ule wa awali kumalizika, hivyo tunaongeza mwingine.

“Yanga nao walionyesha kumhitaji lakini kuna vitu walishindwa kukamilisha na tulipozungumza na Simba wamekubali kurekebisha baadhi ya vipengele, hivyo atabaki huko,” alisema Kisongo.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot