Wajenga sekondari kunusuru wanafunzi, Simba Serengeti - ISSRADHANS

Umoja na uzalendo

Umoja na uzalendo

Hot

Post Top Ad

Your Ad Spot

Monday, 11 December 2017

Wajenga sekondari kunusuru wanafunzi, Simba Serengeti



NA AHMED MAKONGO, BUNDA

Image result for mkuu wa wilaya ya Bunda, Lydia Bupilipili,
Mkurugezi wa halmashauri ya mji wa Bunda, Janeth Mayanja akifafanua jambo(pichani) 



WAZAZI na watu wengine wa kijiji cha Migungani Kata ya Bunda Stoo, mkoani Mara wameungana kujenga shule ya sekondari karibu na makazi yao ili kuwanusuru kuliwa na wanyama wakali wanafunzi wanaoishi mbali na shule.

Wakizungumza na gazeti hili, baadhi ya wazazi walisema ili kutumiza mpango huo wamekubaliana kuchangishana kiasi Shilingi 121,000 kila kaya.
Walisema Kata ya Bunda Stoo ni kati zilizoko karibu na hifadhi ya Taifa ya Serengeti. 

JamboIlielezwa kuwa mkuu wa wilaya ya Bunda, Lydia Bupilipili, ndiye aliyehamaisha ujenzi huo na kuelekeza eneo la ujenzi.
 “Nami nawahamasisha kila mmoja kuwekeza kwenye elimu badala ya mambo mengine ambayo hayana manufaa kwa maisha ya baadaye ya watoto wenu,”alisema wakati alipotembelea kijijini hapo.

Mkurugezi wa halmashauri ya mji wa Bunda, Janeth Mayanja, alisema kuwa kutokuwepo kwa sekondari katika kata hiyo ni changamoto kubwa na kuwataka wananchi, wakiwamo wafugaji katika eneo hilo kuendelea kuchangia nguvu zao kufanikisha ujenzi huo haraka ili ikiwezekana masoko yaanze mwakani.

 Nao baadhi ya wananchi wa kata hiyo walielezea furaha yao kutokana na kuanza kwa ujenzi wa sekondari hiyo, wakisema kuwa watoto wao wametaabika kwa kipindi kirefu kwa kutembea umbali mrefu, huku wakikumbana na changamoto ya kushambuliwa na wanayama wakali.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot