Ripoti mgogoro wananchi, Azam kukabidhiwa serikalini - ISSRADHANS

Umoja na uzalendo

tanzania

Post Top Ad

Monday, 11 December 2017

Ripoti mgogoro wananchi, Azam kukabidhiwa serikalini

Your Ad Spot

6
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga,Mkoa wa Pwani, Mhandisi Mshamu Munde akisalimiana na baadhi ya wananchi wa mwandege,

NA YUSUPH MWAMBA, MKURANGA
MGOGORO kati ya mwekezaji, Kampuni ya Azam na  baadhi ya Wananchi wa Kijiji cha Mwandege, Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga mkoani Pwani huenda ukafikia kikomo baada ya halmashauri  hiyo kumaliza uandikishaji wa Wananchi wanaodai fidia dhidi ya mwekezaji huyo.

Akizungumza na Raia Tanzania, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mkuranga Mkoa wa Pwani, Mhandisi Mshamu Munde, alisema hatua iliyoba ni  kukabidhi ripoti ya mapendekezo kati ya pande mbili , Baraza la Taifa la Usimamizi naUhifadhi wa Mazingira (NEMC) na Halmashauri  kwenda  Ofisi ya Makamu wa Rais, Mazingira iliyotaka ripoti hiyo.

Akifafanua, Mkurugenzi huyo aliwataka Wanakijiji hao kuwa wavumilivu wakati huu serikali ikikamilisha taratibu zilizoshauriwa na kuwahakikishia kuwa kila anayestahili atapewa haki yake.
 
3
Naibu Waziri  wa Mazingira na Muungano, Luhaga Mpina akitaja sababu.
Hata hivyo alikiri kuchelewa kwa taarifa hiyo nje ya muda wa siku 14 zilizotolewa na aliyekuwa Naibu Waziri  wa Mazingira na Muungano, Luhaga Mpina akitaja sababu mbalimbali  ukiwamo uchunguzi wa kina kuhusiana na mgogoro wenyewe kuchukua muda mrefu.

Sababu nyingine ni kubaini kiini cha mgogoro ambapo katika uchunguzi huo ilibainika kuwa malalamiko yamegawanyika, wanakijiji kadhaa wanamlalamikia mwekezaji huyo kutiririsha maji yenye viambata vya kemikali kwenye maeneo yao, kelele na harufu mbaya.
.com/blogger_img_proxy/
Wakati wengine  wanadai nyumba zao zao kumoboka kutokana na maji yanayotiririka kutoka kiwandani humo, alisema.
Mmoja wa wanakijiji hao, Said Mkawala alisema wanaishi kwenye eneo hilo kwa miongo kadhaa ingawa mwaka 2009  Kampuni ya Azam ilijenga kiwanda karibu na makazi yao kabla ya kuanza uzalishaji mwaka 2010 na kutokea kwa madhara hayo.
 “Naibu waziri wa Mazingira alikuja  hapa Oktoba 2017 baada ya kusikia kero zetu za muda mrefu , akakutana na mwekezaji baada ya kutoka maagizo yaliyowafikia viongozi wetu ni kwamba ndani ya siku 14 kuwe na maafikiano ili suluhisho lipatikane, lakini hadi sasa hakuna kinachoendelea. Ikumbukwe tumesimamishwa kufanya shughuli zetu hadi muafa wa suala hili, sisi tupo tayari kulipwa fidia na kuondoka kuliko hali hii,”alisema akiwakilisha wenzake 39.

Kwa mujibu  kifungu  57 (b) (i) cha sheria ya Mazingira  namba 20 ya mwaka 2004  hairuhusiwi kujenga mradi wowote ndani ya mita 200 kutoka makazi ya watu bila ruhusa maalumu , tathimini ya mazingira (EIA) kufuatwa.
Hata hivyo Mkurenzi, Munde alisema taratibu zote za mazingira zilizingatiwa wakati wa ujenzi wa kiwanda hicho mwaka 2009.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad