NA
YUSUPH MWAMBA
TIMU ya Soka ya Kinondoni Municipal Council (KMC),
yenye maskani yake Wilaya ya Kinondoni imeandaa kongamano rasmi kwa ajili ya kuwapongeza
wachezaji wake mara baada ya kufanikiwa kukata tike ya kupanda Ligi kuu Tanzania bara msimu ujao.
Kongamano hilo linatarajiwa kufanyika tarehe 9 mwezi
Februari, 2018 Siku ya Jumamosi kwenye
Uwanja wa Biafra kuanzia majira ya saa 8:oo
mchana.
Akizungumza na mwandishi, Mwenyekiti wa Klabu hiyo, Suzan Massawe, alisema kongamano hilo ni moja ya furaha na
hamasa kwa timu ya KMC kupanda ligi kuu bara kwani wataongeza morali ya ushindani
na hali ya kujituma.
Alisema kongamano hilo linatarajia kuanza mishale ya saa 6 mchana ambapo gari la
matangazo litazunguka na wachezaji wa KMCkatika meneo mbali mbali ndani ya
wilaya ya Kinondoni kisha saa 8 mchana watawasili Uwanja wa Biafra
tayari kwa kukamilisha kongamano hilo.
“Huu ni
utaratibu, tunawapongeza sana KMC kwani walifanya kile tulichowatuma wametubeba
hatuna budi ya kuwapongeza jambo ambalo litawapa morali ya ushindani na hali ya ushindi
watakapoingia kwenye kivumbi cha ligi kuu msimu ujao”, alisema Suzan
Naye Mwenyekiti na mmiliki wa Timu ya soka ya Kinondoni
FC, Saleh Alawi, aliwapongeza KMC na
kuwataka wajenge ushirikiano imara na
kujengeka kifikra katika kuelekea kwenye kinyang’anyiro cha Vodacom ambako
kunaonekana kuwa na ushindani mkubwa tofauti na ligi daraja la kwanza.
KMC ambayo ilikuwa kundi C ilifanikiwa kupanda ligi
kuu baada ya kujikusanyia alama 28 ikifuatiwa na Biashara ya Mara.
No comments:
Post a Comment