Jamii yahamasishwa kula vyakula vya asili - ISSRADHANS

Umoja na uzalendo

tanzania

Hot

Post Top Ad

Monday, 11 December 2017

Jamii yahamasishwa kula vyakula vya asili

Your Ad Spot


 1498473439_004023_1498473691_noticia_normal
NA PETER MWAMKAMBA NA ODRIANI NICOLAUS
JAMII imeshauriwa kula vyakula vua asili ili kuepuka madhara yanayotokana na ulaji holela wa vyakula vyenye viambata vya kemikali na kuwa kwenye hatari ya kupata magonjwa  ambayo hutumia gharama kubwa kujitibu.

Uhauri huo ulitolewa na mjasiriamali na mzalishaji wa vyakula kwa mfumo wa asili wa siku nyingi jijini Dar es Salaam, Yohana Sefue wakati akizungumza na gazeti hili lililotaka kufahamu juhudi za wazalishaji wa bidhaa za  vyakula katika kupunguza tatizo la magonjwa yasiyokuwa ya kuambukiza ambayo sehemu kubwa husababishwa na ulaji wa vyakula vyenye kemikali.

Alisema wakati umefika sasa kwa Watanzania kubadili mfumo wa ulaji, kusikiliza na kutii ushauri wa wataalamu na kusema kuwa ni jamii yenyewe inaweza kuamua namna ya kula  ingawa ni wajibu wa wataalamu kutoa elimu kwao.

“Wakati wote huwa naamini kwamba kila ulacho `ndio wewe’ kwa maana kwamba mtu mwenyewe huamua ale nini kwa faida yake mwenyewe kiafya. Je,  unapoamua ule nini, unatafakari nini sahihi kula kulingana na maelekezo ya wataalamu,?”alihoji.

Alisema magonjwa yasiyokuwa ya kuambukiza kama saratani, kisukari, shinikizo la damu, utapia mlo mkali (savior malnutrition) na magonjwa mengine ya mfumo wa chakula huweza kuzuilika ikiwa watu watakula kwa wingi vyakula vya asili vinavyoelekezwa na wataalamu.

Sefue vyakula hivyo yakiwamo matunda yalizalishwa kwa njia za asili vina sifa nyingine ya kujenga akili, kukinga mwili dhidi ya maradhi na mfumo wa damu mwiliki kufanya kazi ipasavyo.

Aliongeza kwa kuishauri jamii kula vyakula vilivyotengeneza kwa unga wa nafaka vyakula zisivyokobolewa kama vile mahindi, ngano, ulezi na soya. “Hakuna sababu ya kwua na watoto wenye utapia mlo. Kuendelea kwa ugonjwa huo katika jamii, ni ishara kwamba vyakula vinavyotengezwa havitumiki au kutumika kwa kusuasua,”alisema.

Alisifu juhudi za serikali kusimamia masuala ya afya hapa nchini na kushauri mamlaka kuendelea kutoa elimu zaidi kuhusu lishe bora ili kupunguza tatizo la magonjwa yasiyokuwa ya kuambukiza.

Hiyo ni pamoja na kupanua wigo wa kilimo cha mazao yanayotumika kutengeneza bidhaa za asili ili kuwepo kwa mali ghafi ya kutosha kutengeneza vyakula hivyo. Pia kuhamasisha viwanda kuzalisha vyakula hivyo ili kutosheleza katika matumizi.

Takwimu za wataalamu zinaonyesha kuwa asilimia 10 ya Watanzania wanaugua ugonjwa wa kisukari huku asilimia 20 wakisumbuliwa na maradhi ya shinikizo la damu (presha).Pia takwimu zinaonyesha kuwa asilimia 42 ya watoto chini ya miaka mitano wamedumaa wakati asilimia 16 walipoteza maisha na 21 kuzaliwa wakiwa na uzito wa chini.

Utaopiamlo na udumavu wa akili vimeonakana kuishutua serikali na kuamua kuondoa kodi kwenye vitamini, virutubishi na dawa za kusafisha maji ya kunywa ikiwa ni mkakati wa kuimarisha afya ya jamii

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad