
UMOJA
wa
katiba ya wananchi (UKAWA ) nchi umesema
kuwa umejiridhisha kuwa Serikali ya awamu ya Tano sio serikali ambayo inafuata
utawala bora, kuzingatia haki za binadamu huku ikivunja katiba.
Akizungumza na waandishi wa habari, Mwenyekiti mwenza wa Umoja huo, Freeman Mbowe amesema vipo viashiria vingi vinavyoonesha kuwa uongozi wa awamu ya Tano hauzingatii katiba ikiwemo kuzuia mikutano ya kisiasa Pamoja na kushambulia kwa viongozi wa vyama vya upinzani.
" Serikali inabana wazi kuzungumzia na kuikosoa, hata nyinyi wandishi hampo Salama, ndio maana mwenzenu Azory mpaka sasa hajapatikana na serikali haijatoa tamko lolote" amesema Mbowe.
Aidha Mbowe pia alizungumzia uchaguzi mdogo wa madiwani ambapo Kata 43 zilifanya uchaguzi huku CCM, ikishinda Kata 42 na Chadema walishinda moja.
Alisema viongozi wao wakiwemo wabunge, madiwani na wagombea wa upinzani walikua wakikamatwa na kuwekwa ndani huku wasimamizi wao wakitolewa nje ya vyumba vya Kura jambo ambalo ni kinyume na katiba ya nchini.
Akizungumza na waandishi wa habari, Mwenyekiti mwenza wa Umoja huo, Freeman Mbowe amesema vipo viashiria vingi vinavyoonesha kuwa uongozi wa awamu ya Tano hauzingatii katiba ikiwemo kuzuia mikutano ya kisiasa Pamoja na kushambulia kwa viongozi wa vyama vya upinzani.
" Serikali inabana wazi kuzungumzia na kuikosoa, hata nyinyi wandishi hampo Salama, ndio maana mwenzenu Azory mpaka sasa hajapatikana na serikali haijatoa tamko lolote" amesema Mbowe.
Aidha Mbowe pia alizungumzia uchaguzi mdogo wa madiwani ambapo Kata 43 zilifanya uchaguzi huku CCM, ikishinda Kata 42 na Chadema walishinda moja.
Alisema viongozi wao wakiwemo wabunge, madiwani na wagombea wa upinzani walikua wakikamatwa na kuwekwa ndani huku wasimamizi wao wakitolewa nje ya vyumba vya Kura jambo ambalo ni kinyume na katiba ya nchini.
No comments:
Post a Comment