Mfanyabiashara atoa msaada kwenye sekta ya elimu na afya - ISSRADHANS

Umoja na uzalendo

Umoja na uzalendo

Hot

Post Top Ad

Your Ad Spot

Tuesday, 21 November 2017

Mfanyabiashara atoa msaada kwenye sekta ya elimu na afya




NA MWANDISHI WETU, MWANZA

MFANYABIASHARA mmoja  ambaye ni mzaliwa wa wilayani Kwimba mkoani Mwanza, ametoa msaada wa vitu mbalimbali wenye zaidi ya shilingi milioni 27, kwenye sekta ya afya na elimu katika wilaya hiyo, kama fadhira yake akiwa mmoja wa wazawa wa wilaya hiyo.

Mwananchi huyo Richard Mchele, alitoa msaada huo juzi ambao ni pamoja na madawati katika shule tatu za msingi, ujenzi wa vyumba vinne vya madarasa katika shule mbili za msingi, ujenzi wa vyoo viwili vyenye matundu manane ya wasichana na wavulana, pamoja na mifuko 100 ya saruji kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya.

Wakipokea msaada huo kwa nyakati na maeneo tofauti, wananchi, walimu, viongozi pamoja na wanafunzi walimshukuru mwananchi huyo  kwa kukumbuka kwao na kuamua kutoa msaada huo.         

Sostenes Shibula ni mwenyekiti wa kati ya shule ya msingi Nyashana, pamoja na Vicent Mulesa ambaye ni mwalimu mkuu msaidizi wa shule hiyo ni kati ya wananchi waliotoa shukuruani zao kwa mwananchi huyo.

Walisema kuwa afya za wanafunzi zilikuwa hatarini kwa sababu ya shule hiyo kukosa vyoo na kwamba nusura ifungwe kwa sababu ya changamoto hiyo.

“Msaada aliotupatia huyu ndugu yetu tumeupokea kwa mikono miwili, maana afya za watoto wetu zilikuwa mashakani maana hakukuwa na choo na serikali ilikuwa inataka kuifunga” alisema Sostenes Shibula.         

Akikabidhi msaada huo Richard Mchele, alisema kuwa lengo lake ni kusaidia kule alikotoka, huku akiitaka jamii kushirikiana naye katika kuboresha elimu na kuunga mkono juhudi zinazofanywa na rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Joseph Pombe Magufuli katika masuala mbalimbali, ikiwemo sekta ya elimu.

Mchele alisema kuwa aliamua kutoa msaada huo nyumbani kwao kwa sababu ndiko alikozaliwa na kwamba pia hatua hiyo nikuunga mkono juhudi za rais Magufuli katika kuletea wananchi maendeleo.

“Huku ndiko kwetu hivyo nimeamua kutoa msaada huu, ambao wote umegharimu zaidi ya shilingi milioni 27, nikiunga mkono juhudi za rais wetu katika suala zima la kuletea wananchi maendeleo hususan katika sekta ya afya na elimu” alisema.

Mmoja wa wenyeviti wa vijiji ambavyo vimefaidika na msaada huo, Mahenge Joseph, alisema kuwa msaada huo ni mkombozi kwao na kuomba wananchi wengine wenye kipato kuiga mfano wa mfanyabiashara huyo.

Mfanyabiashara huyo pamoja na wenzake wamekuwa na tabia ya kutoa misaada ya kijamii katika mikoa ya kanda ya ziwa, kama fadhira yao kwa kukumbuka kule waliokozaliwa.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot