NA ISSA RAMADJHANI,
KARIBU mwanandoa katika safu ya saikolojia,
tubadilishane mawazo na kujuzana mambo kadhaa kama wanandoa na wachumba.Leo tutazungumzia
tiba kwa majeruhi wa mapenzi mke au mume kusaliti ndoa husababisha kubaki na
maumivu moyoni.
Siku za hivi karibuni wanandoa au wachumba wengi wamekuwa
wakisalitiana na kuvunjika kwa ndoa nyingi,mahusiano kwa hakika tabia hii
inakua kwa kasi na kuona kama jambo la kawaida, ingawa wanasaikolojia wanasema uaminifu
ni silaha kubwa kwa wanandoa
(wapenzi), mbali na mila ,tamaduni katika nchi au jamii na mengine.
Imekuwa ni kwawaida sasa ndoa nyingi kuvunjika au
wachumba kuachana kwa sababu kadhaa yafuata ni muhimu kuyajua na kufanyia kazi
baada ya kuachana na mpenzi wako au
mchumba kuwa faraja ya moyo.
| wapenzi walioacha , |
Mwachie
Mungu na kubali yote yaliyotokea yapite.
Usiruhusu mawazo yatawale kichwani mwako pindi
unapoachan na mpenzi wako wa dhati na isiwe adhabu (maumivu) ,akilini mwako
utajiona kama huna thamani na kuanza kujitoa kasoro kwa kujiuliza maswali mengi
mfano sikumridhisha, sina mvuto na mambo mengi utafikiria.
Kipindi hiki unashauriwa kufunga mlango kabisa kwa ex wako , kwa kufanya maombi kumuomba mungu upate mwingine na ikubali hali hiyo ipite kuanza ukurasa wa maisha mengine ya furaha huku ukimuomba Mungu sana na kusahau yote yaliopita.
Usikumbuke
yaliopita mkiwa pamoja.
Tafuta kitu cha
kufanya ili kukuweka bize muda wote kama mwajiliwa seikali au umejiajiri na wakati
mwingine soma vitabu vya namna ya kufanya ili kupata maendeleo,Angalia tamthilia
mbalimbali ,isipokuwa za mapenzi achana nazo. Ikibidi jitaidi kutafuta marafiki wazuri wa kutoka nao pamoja sehemu za burudanina kwa kufurahi
pamoja.
Epuka kukumbuka ya nyuma yote ya mpenzi wako jinsi mlikuwa mnafanya na kuishi naye pamoja , labda sasa anafanyaje na mwingine, achana na hayo mawazo kabisa .
Husababisha maumivu badala yake utaumia. Hakikisha unakaa muda wa kutosha ili kutafakili akilini mwako, kwa ajili ya kufanya mambo mengine yanayostahili maendeleo ya maisha yako. lakini ukirudisha mawazo ya nyuma sio utaumia tu bali hata wale wanaokuzunguka watashindwa kukusaidia.
Usianzishe
mahusiano mapya kwa kukurupuka.
Kosa watu wengi wakiachika
kwenye mahusiano hukimbilia kutafuta mpenzi mpya ndani ya muda mfupi tu ili kumuonesha ex wake
kuwa na yeye anapendwa kumbe hajui hata huyo aliyempata kwa muda mfupi wahadumu
nae muda mfupi na kujikuta akiachana kila uchwao.
waswahili wanasema ukiwa na furaha sana usichukue maamuzi na hata ukiwa na huzuni usifanye hivyo ni busara kutulia na muombe Mungu na mengine utafanikiwa tuu.
Nitumaini kwa wewe ambaye bado unaugulia maumivu ya kuachwa ukizingatia haya utakuwa umepata faida wapi kwa kuanzia na kurudisha furaha na tabasam iliyokuwa imepotea.
waswahili wanasema ukiwa na furaha sana usichukue maamuzi na hata ukiwa na huzuni usifanye hivyo ni busara kutulia na muombe Mungu na mengine utafanikiwa tuu.
Nitumaini kwa wewe ambaye bado unaugulia maumivu ya kuachwa ukizingatia haya utakuwa umepata faida wapi kwa kuanzia na kurudisha furaha na tabasam iliyokuwa imepotea.
Epuka kutuma
meseji au kumfuatilia ex wako.
Jitahidi usimtumie meseji za kimahaba au ujumbe katita simu mfano
samahani, pole, nimekosea namba kwa mpenzi wako uliye achana naye na punguza kuongea nae ikibidi acha hadi
akutafute mwenyew kwa maana kitendo cha kummtafuta utakuwa unaongeza chumvi
kwenye jeraha lako mwenyewe.
Kwasasa kutokana na utandawazi uliopo ni vyema ukampa (Block) mitandaoni,namba yake ya simu ili kusiwe na mawasiliano hii itakufanya umtoe kichwani kirahisi kwani kitendo cha kumfuatilia mitandaoni kitakuumiza zaidi hebu fikiria wewe usiku mzima hujalala kutokana na maumivu ya kuachwa halafu asubuhi unaingia tuu Instagram unakutana na picha ya ex wako kaposti picha ya Mwanamke/Mwanaume mzuri halafu kaweka emoji ya vikopa kopa hapo lazima urudi kitandani uendelee kulala kuwa bize na mambo yako.
Kwasasa kutokana na utandawazi uliopo ni vyema ukampa (Block) mitandaoni,namba yake ya simu ili kusiwe na mawasiliano hii itakufanya umtoe kichwani kirahisi kwani kitendo cha kumfuatilia mitandaoni kitakuumiza zaidi hebu fikiria wewe usiku mzima hujalala kutokana na maumivu ya kuachwa halafu asubuhi unaingia tuu Instagram unakutana na picha ya ex wako kaposti picha ya Mwanamke/Mwanaume mzuri halafu kaweka emoji ya vikopa kopa hapo lazima urudi kitandani uendelee kulala kuwa bize na mambo yako.
Epuka
kumsema vibaya ulieachana naye.
Mwenza wako anapoamua
kuondoka na kwenda kwa mwingine usiwaambie marafiki zako kuhusu mabaya yake
kwani itakufanya uonekane mtu mbaya bila wewe kujua, utaharibu mwonekano wako
na tabia yako, ukimsema vibaya kuhusu yeye, pia wewe utaonekana ujitetea kuwa mkosaji,
maana wakosaji bila kujiongelea mabaya yake, ndio huongea mabaya ya mpenzi wako
kwa wale ambao hawakufanikiwa.
Epuka
kusikiliza nyimbo za huzuni au kubembeleza.
Baada ya kupigwa
chini au kuachana na mpenzi wako,epuka kusikiliza nyimbo za huzuni au mapenzi
zenye kubembeleza hizi hasababisaha ufikirie majanga yaliyokukuta badala yake
sikiliza nyimbo za kufurahisha zenye kuchezeka na zenye kukufanya ujione wewe
ni mshindi muda wote na mwenye furaha pia jichanganye na watu.
Suluhu fanya maauzi
kwa kumtafuta mpenzi baada ya kupata
ushauri kwa wataalamu wa mahusaiano, wahenga(watu wazima) juu ya mapenzi ,ili
kumpata mpenzi sahii kwa kuzingatia vigezo vyako ambavyo ulituma awali kumpata
mpenzi mpya. Mshirikishe mungu akuongoze
katika mahusiano yako akusimamie
na chagua mwanamke mwenye kariba nzuri, mwelevu pamoja na dini madhubuti.
No comments:
Post a Comment