Siri ya kuwa na meno yenye afya, imara - ISSRADHANS

Umoja na uzalendo

Umoja na uzalendo

Hot

Post Top Ad

Your Ad Spot

Thursday, 26 October 2017

Siri ya kuwa na meno yenye afya, imara


Na Peter Mwamkamba



MENO ni kiungo muhimu kwa maisha ya kia binadamu, hata hivyo kuna aina nyingi ya utunzaji wa kinywa chako ili kisitoe harufu mbaya pamoja na kuyafanya kuwa imara zaidi.

Leo Daktari kutoka nchini India anayeshughulikia tiba ya meno, Meet Ramatri, anafafanua njia bora za utunzaji bora wa kinywa na meno yako.

Dokta Ramatri 



Anasema osha meno yako mara mbili kila siku. Tumia uzi ili kusafisha maeneo ambayo hayafikiwi na mswaki ili kuondoa  uchafu kwenye maeneo yanayounganisha jino moja na lingine.



Aidha, anasema futa kinywa chako kabisa baada ya kula chakula chochote. Hii itafuta au kuondoa mabaki ya chakula ambacho kinapatikana kwenye sehemu za meno na pia hupunguza uchafu unaotokana na rangi ya chakula kwenye meno.

Anashauri kutumia mswaki wenye dawa ya meno ili kuondoa vipande vilivyopo kwenye meno na uchafu wa chakula ambao umekusanywa ndani ya meno.

 
Pia anasema punguza ulaji wa chakula kinachoweza kufanya kinywa chako kuwa safi kwa muda mdogo, kupunguza ulaji wa chakula laini na kichafu a kwamba vyakula vitamu (vyenye sukari) huwa vinakaa kwenye meno kwa muda mrefu hasa juu ya meno na kuanzisha kuoza kwa jino.

Anashauri kuiwekea utaratibu wa kusafisha fizi mara kwa mara, kumia chakula cha afya kilicho na wingi wa protini, vitamini na kalsiamu.

Ansema matumizi ya dawa ya meno ya fluorid husaidia kudhibiti uharibifu wa jino

kwa watoto wadogo, hivyo ni vizuri kutumia mswaki wenye dawa ya meno wenye nyuzi zenye uwezo wa kupenye sehemu za wazi au mashimo ya kudumu na fika kwa mtaalam wa meno mara moja kila baada ya  miezi minne au sita kwa uchunguzi wa kawaida.



EPUKA YAFUATAYO

Dokta Ramatri anashauri ili kulinda meno yako na kuyafanya kuwa imara epuka sigara kwani husababisha meno yako kuoza.

Aidha anasema epuka matumizi ya vinywaji vya kusindika ambavyo vinaweza kufuta tabaka la meno na epuka kula chakula kigumu sana ambacho kinaweza kusababisha kuvunjika kwa meno.



Anashauri kujiwekea tabia kama kusaga au kuunganisha meno yako wakati wa usiku ambayo inajulikana kama bruxism ambayo huzuia kuenea kwenye uso wa meno. Hii inazuia  kutoboka au kufanya meno yabadilike katika hali isiyo ya kawaida, kuvaa meno na kuhakikisha yanadumu kwa muda mrefu pamoja  na viungo vya taya.

IDW (India Dental World)





No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot