Na Mwandishi wetu.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna
Mstaafu Zelote Stephen ameziagiza Halmashauri zote zilizopo Mkoani kwake
kuhakikisha wanakuwa na magulio rasmi ya kuuzia mahindi ili, wakulima na wafanyabiashara
waweze kufuata utaratibu .
![]() |
| Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen pichani |
husika zinazosimamia uingizwaji wa bidhaa kutoka katika nchi za jirani.
"Ni mategemeo yangu kuwa wakurugenzi wataanzisha vituo ili wakulima waweze kupeleka mazao yao hapo na kuweza kuyauza na ndipo nao halmashauri waweze kukusanya ushuru unaotakiwa, lakini hizi biashara zinazofanywa kupitia njia za panya, nasema si kitu cha kuachiwa, hivyo basi nisingependa kuona malori yanaruhusiwa kwenda maeneo ambayo siyo mipaka rasmi kuchukua mizigo na kuingiza nchini," Amesema.
Na kuongeza kuwa hakuna tatizo kufanya biashara na nchi za jirani isipokuwa biashara hizo zifanywe kihalali kwa kufuata sheria zilizowekwa na chi husika .
Akifafanua Mh. Zelote Alisema kuwa Mkoa wa Rukwa una mahindi ya kutosha na wafanyabiashara wa mikoa mingine wafike kununua na sio kuvuka mipaka kwa njia za panya kufanya biashara hiyo.
Kwa upande wao wafanyabiashara waliohojiwa na Mh. Zelote katika ziara yake hiyo walidai kuwa mahindi yanayotoka Zambia bei yake ni nafuu zaidi kuliko ya Tanzania lakini pia wakulima wa Tanzania huficha mahindi yao wakisubiri kupanda kwa bei jambo ambalo ni hasara kwa wafanyabiashara wanaotoka nje ya Mkoa wa Rukwa.

No comments:
Post a Comment