NA ISSA RAMADHANI.
KARIBU msomaji
wangu katika safu hii ya saikolojia. Ni siku nyingine tena kwa neema yake Mungu
amejaalia tubadilishane mawazo na kufahamishana mambo kadhaa muhimu katika maisha yetu ya kila siku.
Leo tutazungumzia sababu za wanaume kufa mapema kuliko
wanawake katika ndoa au uchumba.
Utakubaliana na mimi kwamba wanaume wengi walioko
kwenye ndoa wanakufa mapema na kuwaacha wake au wachumba wao wakiwa katika hali
ya huzuni na majonzi.
Ni mipango ya Mungu binadamu kufa lakini wakati
mwingine sisi binadamu wenyewe hujisababishai au kusababishiwa kifo bila kujua
au kwa kujua.
Kisaikolojia baadhi ya wanaume walioko kwenye ndoa hufa
mapema na kuwaacha wake au wapenzi na familia. Hapa nitaeleza baadhi ya chanzo
cha wanaume kufa mapema kuliko wnawake katika ndoa.
MSONGO
WA MAWAZO
Wanaume ndio waathirika wakubwa wa tatizo la msongo wa mawazo (stress), ingawa kwa nje wanajitahidi kuonyesha kuwa mambo yako shwari wakati wanatafunwa ndani kwa ndani.
Wanaume ndio waathirika wakubwa wa tatizo la msongo wa mawazo (stress), ingawa kwa nje wanajitahidi kuonyesha kuwa mambo yako shwari wakati wanatafunwa ndani kwa ndani.
Utafiti mdogo unaonyesha wanaume hospitalini
wanaokufa kwa presha ya kupanda au ya kushuka, kiharusi, moyo kusimama, kupasuka
kwa mishipa ya damu, matatizo ya mifupa
au maimivu ya kichwa chanzo kikubwa ni msongo wa mawazo.
USIRI
Wanaume wengi ni wasiri, ni wagumu kueleza au kuweka
wazi yanayowasibu na kubakia kuugulia moyoni.
Wengi hawapendi kuwashirikishi watu wengine matatizo
yaliyopo katika ndoa zao hata pale yanapokuwa sugu na kuwafanya waishi bila ya
amani huku wakiwa na msongo wa mawazo usioisha.
Wako tayari wafe na tai shingoni wakijifanya
hawaumii au hawana tatizo.
Baadhi ya wanaume wakiwa na tofauti kwenye ndoa zao zao wakaitwa sehemu
kuyaongea ili kupata ufumbuzi pale zinapokuwa nje ya uwezo wao, huwawapati, anaweza
kukwambia mambo yetu tutasuluhisha wenyewe wakati ndani kwa ndani yanamla na
hatimaye kummaliza kiafya na hata kusababisha kifo.
KUTOJALI AFYA
Ni rahisi sana mwanaume akajisikia vibaya asiende hospitalini kwa wakati kuangalia afya yake tofauti na mwanamke.
KUTOJALI AFYA
Ni rahisi sana mwanaume akajisikia vibaya asiende hospitalini kwa wakati kuangalia afya yake tofauti na mwanamke.
Hata pale anapohimizwa kwenda anaweza kukwepa au kuwa
mbishi au hata kudanganya ameshakwenda au ameshakunywa dawa kumbe mwongo.
Tabia hii husabaisha
ugonjwa kuwa mkubwa na husababisha kifo kwa uzembe wa kujali afya.
KUTOSAMEHE
Kusamehe sio tu kwa faida ya anayesamehewa bali pia kwa afya yako unayesamehe. Mzigo unaoutua kutokana na kusamehe huondoa maumivu moyoni na kumaliza msongo wa mawazo.
Kusamehe sio tu kwa faida ya anayesamehewa bali pia kwa afya yako unayesamehe. Mzigo unaoutua kutokana na kusamehe huondoa maumivu moyoni na kumaliza msongo wa mawazo.
Baadhi ya wanaume ni wagumu sana kusamehe. Wako
tayari wayabebe moyoni matatizo kwa miaka
hali amabyo inawamaliza bila wao kujua.
TABIA
HATARISHI
Wanaume wengi kwenye ndoa wanaoongoza kushiriki tabia hatarishi kama vile ulevi, anasa, ngono holela na tabia hizi huwaweka karibu zaidi na jeneza kuliko wake zao wanaowaacha nyumbani.
Wanaume wengi kwenye ndoa wanaoongoza kushiriki tabia hatarishi kama vile ulevi, anasa, ngono holela na tabia hizi huwaweka karibu zaidi na jeneza kuliko wake zao wanaowaacha nyumbani.
Kibaya zaidi
hata wanapopata maambukizi ya magonjwa, watoto wa nje ya ndoa huwadanganya
hawawaambii ukweli wenza wao na kusababisha matatizo makubwa zaidi katika
familia.
No comments:
Post a Comment