Serikali iwekeze nguvu usimamizi wa dawa za Mifugo - ISSRADHANS

Umoja na uzalendo

Umoja na uzalendo

Hot

Post Top Ad

Your Ad Spot

Wednesday, 25 October 2017

Serikali iwekeze nguvu usimamizi wa dawa za Mifugo



NA ODRIAN  NICOLAUS 

SERIKALI imeombwa kupunguza bei za dawa za kutibia mifugo na kusimamia bei elekezeki kipindi dawa zinapofika kwa mawakala hii ni kutokana n kupanda kwa ghrama kila siku na kusababisha huduma kuwa ngumu.

Akizungumza na gazeti hili, Dk. Wa mifugo kutoka mkoani Kilimanjaro, Nicolaus Gerald, alisema kuwa Serikali inatakiwa kutazama upya swla la kupanda kwa gharama za dawa za mifugo kwani ni moja ya sekta ambayo wtu wengi wameamua kujikita katika kujiajiri.

 Aidha, Dk. Gerald alisema wataalamu wa Vijini kwa sasa wanatakiwa kukabilaiana kutokana na mabadiliko ya tabia ya nchi na maendeleo ya Sayansi na Teknolojia na wajenge utaratibu wa kutembeleana kufika katika maeneo husika tofauti na hapo nyuma walikuwa wanakaa ofisini au wakiitwa kipindi matatizo yanapotokea.

Dk. Gerald, alitoa ushauri huku aikiomba Serikali iwatazame kwa karibu wataalamu waliojitolea na kutoa huduma Vijijini kwa kuwasaidia usafiri waweze kutoa huduma kwa urahisi  ikiwamo kutembelea nyumba kwa nyumba wakitoa elimu ya namna bora ya  ufugaji.
 

Dk. Gerald

Mkazi mmoja ambaye anajihusisha na ufugaji wa kuku, Remi Mtei, alisema kuwa anawashukuru wataalamu wa mifugo kwa kujitolea kufundisha elimu hiyo kwani ni faida kwao katika kuendesha maisha yao.

“Kupitia wataalamu binafsi nimefurahi sana kunipatia mifugo yangu chanjo na njia za kisasa za ufugaji, hivyo kil baada ya miezi mitatu wanapokuja wanaturahisishia kutambua vizuri ufugaji pamoja na changamoto zinazotukabili ila sitosita kuwapongeza”alisema Mtei

.Upo umuhimu wa Serikali kutizama matatizo ya Wajasiriamali na wataalamu wanaoamua kujiajiri kwa karibu ili waweze kuleta Taiafa lenye maendeleo na kuamsha ari kwa Vijana wengine kuchangamkia fursa.


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Your Ad Spot